Mercredi 17 juillet 2024

Archives

Waislamu washerehekea Id il Hajj katika mfarakano

05/05/2013 Commentaires fermés sur Waislamu washerehekea Id il Hajj katika mfarakano

Malumbano ni hasa upande wa viongozi wa Jumuia ya kiislamu nchini Burundi COMIBU : kuna kundi la sheikh Sadik Kajandi anayetambuliwa na wizara ya mambo ya ndani na kundi la Al-Haj Haruna Nkunduwiga aliyeteuliwa na baraza kuu la mashehe.

<doc1909|right>« Allah Akbar, Allah Akbar, Allah Akbar, Mwenyezi Mungu ni mkubwa », bada ya takbira hizo na bada ya Imam aliyeongoza swala kutowa hutba yake akiwaomba waislamu kushikamana, Sheikh Sadiki Kajandi, anayezidi kubaini kuwa ndie kiongozi wa Jumuia ya kiislamu nchini Burundi alitolea wito waislamu akiwataka kuzidi kupendana, na kuombea Burundi ipate usalama. Aliwaomba pia kutotega sikio ’’wale wanaotaka kusambaratisha waislamu’’. Kundi hilo aliliomba kutoendelea katika njia hio ’’sababu uislamu ni amani’’. Wapinzani wake hao aliwaomba wasiendeleye kuleta mfarakano na shari baina waislamu. Sheikh Kajandi alionekana akiwa na kundi la watu waliokuwa wakimfuata kwa karibu, ’’pengine ni walinzi wake’’, alisema hayo muumini mmoja bada ya ibada hio.

Ibada yenyewe ilifanyika chini ya ulinzi mkali, kwenye uanja wa COMIBU tarafani Nyakabiga. Kilicho dhahiri ni kua idadi ya askari polisi iliongezwa ikilinganishwa na miaka iliyopita. Kawaida, badhi ya waislamu jijini Bujumpbura hua wanapenda kujumuika kwenye uanja huo wa COMIBU licha ya kua ibada zilifanyika katika tarafa zingine za mji wa Bujumbura kama huko Kibenga tarafani Kinindo, Kanyosha, Buyenzi na Buterere.
Licha ya kua uanja wa Nyakabiga uliandaliwa na Al-Hajj Haruna Nkunduwiga Kiongozi wa jumuia ya kiislamu nchini Burundi, aliyeteuliwa na Baraza kuu la mashehe, akiambatana na waislamu zaidi ya 200, kiongozi huyo wa COMIBU ambae bado kutambuliwa na wizara ya mambo ya ndani na kundi lake walichukuwa uamzi wa kisalia tarafani Buterere. « Uamzi huo umechukuliwa ili kusitokeye vurugu wakati wa ibada sababu ilionekana Kajandi alikuwa na wahuni karibu kumi ambao walikuwa tayari kuvuruga sala walakin hatukuwapa na fursa hio sababu uislamu si diniya mvutano ».

<doc1908|left>Al-Hajj Nkunduwiga anapongeza waislamu kwa kudiriki sala katika hali ya utulivu. Alimtolea wito waziri wa mambo ya ndani aheshimishe sheria kwa kuwatambua viongozi walioteuliwa na waislamu na ’’ikiwa Bw. Kajandi ana sifa fulani ambazo zinamridhisha waziri huyo basi ampe kazi’’, anazidi kusema kiongozi huyo wa Jumuia ya kiislamu nchini Burundi aliyeteuliwa na Baraza kuu la mashehe.

A nos chers lecteurs

Nous sommes heureux que vous soyez si nombreux à nous suivre sur le web. Nous avons fait le choix de mettre en accès gratuit une grande partie de nos contenus, mais une information rigoureuse, vérifiée et de qualité n'est pas gratuite. Nous avons besoin de votre soutien pour continuer à vous proposer un journalisme ouvert, pluraliste et indépendant.

Chaque contribution, grande ou petite, permet de nous assurer notre avenir à long terme.

Soutenez Iwacu à partir de seulement 1 euro ou 1 dollar, cela ne prend qu'une minute. Vous pouvez aussi devenir membre du Club des amis d'Iwacu, ce qui vous ouvre un accès illimité à toutes nos archives ainsi qu'à notre magazine dès sa parution au Burundi.

Editorial de la semaine

Dépités par nos députés

En décembre dernier, une députée a revendiqué, lors d’une séance de questions au ministre de l’Énergie, une station-service réservée uniquement aux élus, se plaignant d’être méprisée lorsqu’elle devait faire la queue. Ces propos ont profondément choqué l’opinion publique et ont (…)

Online Users

Total 3 055 users online