Mardi 16 juillet 2024

Archives

Kiongozi wa mungano wa vyama vya upinzani akamatwa leo alfajiri na kupelekwa mahakamani na askari polisi

20/09/2011 Commentaires fermés sur Kiongozi wa mungano wa vyama vya upinzani akamatwa leo alfajiri na kupelekwa mahakamani na askari polisi

Kwa mujibu wa duru za kuaminika kutoka chama chake cha FRODEBU, Bw. Léonce Ngendakumana ambae pia ni kiongozi wa mungano wa vyama vya upinzani nchini Burundi, ADC-Ikibiri amekamatwa na askari polisi leo alfajiri na wakati huu anahojiwa mahakamani. Duru hizo zasema hata viongozi wengine wa chama hicho cha FRODEBU, wamepewa waranti na wanahojiwa mahakamani pia.

Wakati hayo yakiarifiwa duru zasema hata mwanaharakati wa haki za binadamu, Pierre Claver Mbonimpa, kiongozi wa shirika liitwalo ’’APRODH’’ amepewa waranti hapo usiku wa kuamkia leo na anatazamiwa kuhojiwa pia mahakamani.

Hayo ni bada ya kutangaza bayana kua kuna operesheni iitwayo ’’Safisha’’ambayo ni msako unaoendeshwa na polisi dhidi ya ’’makundi ya wajambazi na wafuasi wa Agathon Rwasa’’, kinara wa zamani wa chama cha waasi cha FNL aliyeamuwa kuingia mafichoni baada ya madai ya uizi wa kura katika uchaguzi wa hapo mwaka jana uliopelekea chama cha CNDD FDD kujinyakulia ushindi.

Si mara ya kwanza mwanaharakati huyo wa haki za binadamu nchini Burundi, kuiitishwa mahakamani kujieleza kuhusu operesheni hio na alibaini kua ’’operesheni hiyo na matamshi hayo si mambo aliyoyazua bali ni maneno kutoka kwa walionusurika katika msako huo unaoendeshwa na polisi. Kiongozi wa shirika hilo liitwalo ’’APRODH’’ anakiri kua ’’walionusurika wanabaini kua waliyasikia yakisemwa na askari polisi wakati wa msako huo ambao unafanyika kwa ushirikiano fika na vijana wakereketwa wa chama tawala cha CNDD FDD”. Madai hayo yanakanushwa na kutupiliwa mbali na kiongozi wa vijana hao, mbunge Ezéchiel Nibigira.

A nos chers lecteurs

Nous sommes heureux que vous soyez si nombreux à nous suivre sur le web. Nous avons fait le choix de mettre en accès gratuit une grande partie de nos contenus, mais une information rigoureuse, vérifiée et de qualité n'est pas gratuite. Nous avons besoin de votre soutien pour continuer à vous proposer un journalisme ouvert, pluraliste et indépendant.

Chaque contribution, grande ou petite, permet de nous assurer notre avenir à long terme.

Soutenez Iwacu à partir de seulement 1 euro ou 1 dollar, cela ne prend qu'une minute. Vous pouvez aussi devenir membre du Club des amis d'Iwacu, ce qui vous ouvre un accès illimité à toutes nos archives ainsi qu'à notre magazine dès sa parution au Burundi.

Editorial de la semaine

Dépités par nos députés

En décembre dernier, une députée a revendiqué, lors d’une séance de questions au ministre de l’Énergie, une station-service réservée uniquement aux élus, se plaignant d’être méprisée lorsqu’elle devait faire la queue. Ces propos ont profondément choqué l’opinion publique et ont (…)

Online Users

Total 3 254 users online