Mercredi 17 juillet 2024

Archives

Gatumba : viongozi wa serekali ya Burundi washiriki misa ya kuomboleza vifo vya watu 39 wa Gatumba

05/05/2013 Commentaires fermés sur Gatumba : viongozi wa serekali ya Burundi washiriki misa ya kuomboleza vifo vya watu 39 wa Gatumba

<doc1399|left>Ibada hio ilikuwa hasa ni katika sherehe za kutinda msiba, kando ya wakaazi wa mtaa wa Gatumba ibada hio ya misa ilihuduriwa na makamo wa pili wa rais Gervais Rufyikiri. Misa hio ilihudhuriwa pia na mawaziri wa serekali ya Burundi pakiwemo waziri wa ulinzi, waziri wa usalama wa raia, waziri wa mambo ya ndani, waziri wa mshikamano wa kitaifa, waziri anayehusika na maswala ya Jumuia ya Afrika Mashariki, waziri wa wafanyakazi wa serekali na msemaji wa serekali. Maseneta na wabunge walishiriki pia sherehe hizo za maombolezi. Katika ibada hizo kulionekana pia mabalozi, Rais wa zamani wa Burundi, Domitien Ndayizeye na mkewe na waakilishi wa mashirika ya kiraia pakiwemo mwanaharakati wa haki za binadamu Pierre Claver Mbonimpa, kiongozi wa shirika la APRODH.

Misa hio ilisomwa na Askofu Anatole Ruberinyange, licha ya kua picha kanisani ilikua haiwezi kufananishwa na ile ya majonzi ya hapo ijuma tatu wakati wa mazishi ya watu hao 39 waliouwawa kikatili, hali ilikuwa ni ya huzuni. Askofu Ruberinyange alisisitiza umuhimu wa mshikamano, umoja na kuheshimu uhai wa kila binadamu.

Katika risala yake makamo wa pili wa rais, Gervais Rufyikiri alikiri kua serekali ya Burundi italifanya kila iliwezalo ili waliohusika kwa njia moja au nyingine katika mauaji hayo ya Gatumba yaliyapelekea watu 39 kuuwawa wakamatwe, wafikishwe mahakamani na waadhibiwe kwa mujibu wa sheria.

Alivikumbusha vyombo vya habari amri iliyotolewa na serekali ya Burundi ya kuvikataza kutowa habari au udadisi kuhusu uchunguzi unaofanyika juu ya mauaji hayo ili ’’uchunguzi huo usipotoshwe’’. Makamo wa pili wa rais, Gervais Rufyikiri aliwaomba raia kushiriki wote kwa ujumla katika mpango wa kuboresha amani na usalama kwa kushirikiana na vyombo vya usalama, vyombo vya sheria na utawala.

Katika hutuba yake, mwaakilishi wa familia za wafiwa aliomba serekali ya Burundi ifuatilie kwa karibu uchunguzi huo unaofanyika ili waliohusika katika mauaji hayo ya Gatumba waadhibiwa vikali. Aliomba pia usalama mtaani humo Gatumba ulindwe ipasavyo. Mwaakilishi huyo wa familia za wafiwa alitolea wito serekali ya Burundi akiitaka ifuatilie kwa karibu hali ya majeruhi wanaolazwa hospitalini. Anasema 2 miongoni mwao itabidi wapelekwe kutibiwa ugenini.

Katika sherehe hizo wizara ya mshikamano wa kitaifa ilijiunga na familia za wafiwa na kila familia ilipewa zawadi au msaada ambao ni pamoja na mchele, maharage, chumvi, jembe vitenge, sabuni na vinginevyo kama ishara kua serekali ya Burundi inashikamana na raia hao wa Gatumba katika msiba huo.

A nos chers lecteurs

Nous sommes heureux que vous soyez si nombreux à nous suivre sur le web. Nous avons fait le choix de mettre en accès gratuit une grande partie de nos contenus, mais une information rigoureuse, vérifiée et de qualité n'est pas gratuite. Nous avons besoin de votre soutien pour continuer à vous proposer un journalisme ouvert, pluraliste et indépendant.

Chaque contribution, grande ou petite, permet de nous assurer notre avenir à long terme.

Soutenez Iwacu à partir de seulement 1 euro ou 1 dollar, cela ne prend qu'une minute. Vous pouvez aussi devenir membre du Club des amis d'Iwacu, ce qui vous ouvre un accès illimité à toutes nos archives ainsi qu'à notre magazine dès sa parution au Burundi.

Editorial de la semaine

Dépités par nos députés

En décembre dernier, une députée a revendiqué, lors d’une séance de questions au ministre de l’Énergie, une station-service réservée uniquement aux élus, se plaignant d’être méprisée lorsqu’elle devait faire la queue. Ces propos ont profondément choqué l’opinion publique et ont (…)

Online Users

Total 2 969 users online